Monday, March 28, 2016

Shein aitisha Baraza la Wawakilishi



 

RAIS wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein ameitisha mkutano wa kwanza wa Baraza jipya la Tisa la Wawakilishi keshokutwa kwenye Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi, Chukwani mjini Unguja.
Hayo yameelezwa na Katibu wa Baraza la Wawakilishi, Dk Yahya Khamis Hamad wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Baraza la Wawakilishi jana.

Hamad alisema amepokea barua kutoka kwa Rais Shein ambayo inaitisha mkutano wa kwanza wa Baraza la Wawakilishi, ambalo kwa mujibu wa kanuni zake, linamtambua Rais kama ni sehemu ya pili ya baraza hilo na ndiyo mwenye mamlaka ya kuamua tarehe na mahala pa kufanyika mkutano wa kwanza.

Alisema kama Kanuni za Baraza la Wawakilishi Toleo la 2012 linaelezea kuwa katika Mkutano wa Kwanza wa Baraza la Wawakilishi shughuli ya mwanzo ni kumchagua Spika wa Baraza la Wawakilishi, na hadi sasa aliyeteuliwa na kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo ambaye amethibitishwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar ni Zuber Ali Maulid kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Katibu wa Baraza la Wawakilishi alisema wajumbe wote wameanza kujengewa mazoea ikiwa pamoja na kujisajili kuanzia leo hadi Aprili 6, mwaka huu. “Kesho (leo) kusajiliwa kwa wajumbe na kupigwa picha za vitambulisho, Machi 29 asubuhi kutakuwa na mkutano wa vyama vya siasa, pia siku hiyo mchana kutakuwa na mkutano wa mwanzo wa wajumbe wote wa baraza, Machi 30 kuanza kwa mkutano wa kwanza wa baraza na baadaye uchaguzi wa spika pamoja na kiapo cha spika na wajumbe,” alisema Hamad.

Aliwaambia waandishi wa habari kuwa Machi 31, mwaka huu kutakuwa na uchaguzi wa Naibu Spika na Mwenyekiti wa Baraza, Aprili 5, 2016 kutakuwa na uchaguzi wa wajumbe wa Tume ya Bajeti ya Baraza na wajumbe watano wa baraza watakaoingia katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Baraza hilo jipya linalotarajiwa kuanza keshokutwa litakalohutubiwa na Dk Shein lina idadi ya wajumbe 88 ambao wajumbe 54 ni wawakilishi waliochaguliwa na wananchi, 22 Wawakilishi wa Viti Maalumu, 10 uteuzi wa Rais ambao bado kuteuliwa, Mjumbe mmoja ambaye ni Mwanasheria Mkuu na Spika ambaye ni nje ya wajumbe wa baraza.

Shein aitisha Baraza la Wawakilishi



 

RAIS wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein ameitisha mkutano wa kwanza wa Baraza jipya la Tisa la Wawakilishi keshokutwa kwenye Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi, Chukwani mjini Unguja.
Hayo yameelezwa na Katibu wa Baraza la Wawakilishi, Dk Yahya Khamis Hamad wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Baraza la Wawakilishi jana.

Hamad alisema amepokea barua kutoka kwa Rais Shein ambayo inaitisha mkutano wa kwanza wa Baraza la Wawakilishi, ambalo kwa mujibu wa kanuni zake, linamtambua Rais kama ni sehemu ya pili ya baraza hilo na ndiyo mwenye mamlaka ya kuamua tarehe na mahala pa kufanyika mkutano wa kwanza.

Alisema kama Kanuni za Baraza la Wawakilishi Toleo la 2012 linaelezea kuwa katika Mkutano wa Kwanza wa Baraza la Wawakilishi shughuli ya mwanzo ni kumchagua Spika wa Baraza la Wawakilishi, na hadi sasa aliyeteuliwa na kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo ambaye amethibitishwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar ni Zuber Ali Maulid kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Katibu wa Baraza la Wawakilishi alisema wajumbe wote wameanza kujengewa mazoea ikiwa pamoja na kujisajili kuanzia leo hadi Aprili 6, mwaka huu. “Kesho (leo) kusajiliwa kwa wajumbe na kupigwa picha za vitambulisho, Machi 29 asubuhi kutakuwa na mkutano wa vyama vya siasa, pia siku hiyo mchana kutakuwa na mkutano wa mwanzo wa wajumbe wote wa baraza, Machi 30 kuanza kwa mkutano wa kwanza wa baraza na baadaye uchaguzi wa spika pamoja na kiapo cha spika na wajumbe,” alisema Hamad.

Aliwaambia waandishi wa habari kuwa Machi 31, mwaka huu kutakuwa na uchaguzi wa Naibu Spika na Mwenyekiti wa Baraza, Aprili 5, 2016 kutakuwa na uchaguzi wa wajumbe wa Tume ya Bajeti ya Baraza na wajumbe watano wa baraza watakaoingia katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Baraza hilo jipya linalotarajiwa kuanza keshokutwa litakalohutubiwa na Dk Shein lina idadi ya wajumbe 88 ambao wajumbe 54 ni wawakilishi waliochaguliwa na wananchi, 22 Wawakilishi wa Viti Maalumu, 10 uteuzi wa Rais ambao bado kuteuliwa, Mjumbe mmoja ambaye ni Mwanasheria Mkuu na Spika ambaye ni nje ya wajumbe wa baraza.

Dk Magufuli: Tusibaguane





RAIS John Magufuli amewataka Watanzania waendeleze upendo na mshikamano walionao ili kuendelea kuilinda amani ya nchi na wasibaguane. Akizungumza wakati wa Ibada ya Pasaka iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) la Azania Front, Dar es Salaam jana, Rais Magufuli alisema Watanzania wanapaswa kutokubaguana kwa dini, rangi wala makabila na washirikiane katika umoja wao.

Rais Magufuli alisema wakati taifa likiadhimisha sikukuu hiyo ya kufufuka kwa Yesu Kristo, wananchi wanapaswa kusherehekea kwa kufanya kazi ili taifa lisonge mbele.
“Niwaombe Watanzania wenzangu wakati tunaadhimisha Sikukuu hii ya kumbukumbu ya kufufuka kwa Yesu Kristo tufufuke naye katika upendo wake lakini tufanye kazi kweli kweli kwa sababu vitabu vinasema asiyefanya kazi na asile,” alisema Rais Magufuli.

Aidha, alisema endapo Watanzania kwa umoja wao wakiamua kufanya kazi kwa bidii, Taifa halitakuwa masikini na kuacha kutegemea misaada ya wahisani wa nje. Alisema kuwa Tanzania ni nchi iliyojaaliwa neema kwa kuwa na rasilimali nyingi na hivyo wananchi wanatakiwa kusimama imara ili iweze kuja kuwa Taifa litakalokuwa likitoa misaada kwa mataifa mengine ya nje.

Rais Magufuli aliwaomba Watanzania kutochoka kuliombea Taifa pamoja na yeye ambaye ana jukumu gumu na zito lakini kupitia maombi ya wananchi anaamini atatimiza yale aliyotakiwa kuyatimiza.

“Naomba Watanzania tusichoke kuliombea Taifa letu, na mimi nawashukuru kwa kuendelea kuniombea. Jukumu hili ni gumu, zito na ni msalaba lakini najua kwa sala zenu, kwa maombi yenu nitatimiza yale ninayotakiwa kuyatimiza,” alieleza Rais Magufuli.

Kwa upande wake, Askofu Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Dk Alex Malasusa aliyeongoza ibada hiyo, aliwakumbusha wananchi kurejesha maadili ndani ya nyumba zao yaliyoanza kupotea kwa kumrudia Mungu.

Askofu Malasusa alisema kuwa fmilia nyingi siku hizi zimeparaganyika, ndoa nyingi zimekuwa hazidumu kwa sababu watu wameacha kufanya ibada na hivyo maadili tena katika nyumba yamepotea. “Tufufue maisha ya uadilifu ndani ya ndoa zetu.

Siku hizi baba na mama wanazikimbia nyumba zao kwa sababu maadili yamepotea ndani ya nyumba, turudishe maadili kwa kufanya ibada,” alisema Dk Malasusa. Aidha, Askofu Malasusa aliwataka Watanzania kwa imani zao kuacha kumsifu Rais Magufuli kwa kupiga makofi na badala yake kila mmoja kwa imani yake asimame na kumuombea kwa kuwa sasa taifa limeanza kuwa na matumaini mapya na nuru kwa kumpata kiongozi aliye mwadilifu.

Saturday, March 12, 2016

Katibu Mtendaji NACTE ajiuzulu


KATIBU Mtendaji wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), Dk Primus Nkwera.

KATIBU Mtendaji wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), Dk Primus Nkwera, amejiuzulu nafasi hiyo ili kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali. Uamuzi wa kujiuzulu kwa Dk Nkwera, ulitangazwa juzi na Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza hilo, Steven Mlote wakati akizungumza na wafanyakazi wa baraza hilo kwenye kikao cha dharura

Mlote alisema, Dk Nkwera amefikia uamuzi wa kujiuzulu, ili kulinda hadhi ya baraza hilo, baada ya gazeti moja la kila wiki kuchapisha habari zikimtuhumu kwa mambo mbalimbali, ikiwemo madai ya kughushi vyeti.
Alisema kwa mujibu wa Dk Nkwera nafasi kubwa kama hiyo katika taasisi ya elimu, haipaswi kushikwa na mtu mwenye tuhuma ya aina yoyote, hivyo baada ya kutafakari ameona ajiweke pembeni na uongozi wa baraza hilo, ili uchunguzi ufanyike akiwa pembeni.

“Tumetumia muda mrefu kutafakari hoja za Dk Nkwera na tumekubali kujiuzulu kwake kwa shingo upande,” alisema Mlote akiwaambia wafanyakazi waliokuwa katika kikao hicho. Mlote alisema kazi iliyofanywa na Dk Nkwera akiwa kiongozi wa baraza hilo inafahamika kwa kila mmoja na uamuzi wake huo ni majonzi kwa baraza hilo.

“Najua mmepata mshituko mkubwa, lakini Dk Nkwera hajafa. Yuko hai, na huyu bado ni mtumishi wa Serikali. Alichofanya ni kuamua kuachana na ukatibu mtendaji. Tutaendelea kumtumia itakapobidi kwa ushauri.

“Wakati mwingine ni lazima mkubaliane na hali hii, lakini endeleeni kuchapa kazi kwa ufanisi kama kawaida, kana kwamba bado mko na Dk Nkwera,” alisema Mlote. Kutokana na kujiuzulu kwa Dk Nkwera, Mlote alieleza kuwa Bodi imemteua Mkurugenzi wa Mitaala wa baraza hilo, Dk Adolf Rutayunga kukaimu nafasi hiyo wakati taratibu nyingine zikiendelea.
Akizungumza katika kikao hicho, Dk Rutayunga alisema kuwa viatu ambavyo ameiacha Dk Nkwera ni vikubwa kwake lakini atajitahidi kuhakikisha anaendeleza yale yote ambayo ameyaacha.
“Jambo hili ni kubwa, uamuzi huu wa kujiuzulu kwa Dk Nkwera ni mzito, lakini hatuna cha kufanya. Tutashikamana kuhakikisha kwamba kazi za Baraza zinasonga mbele kwa weledi uleule” alisema.
Mlote alipotafutwa na mwandishi wetu alikiri Dk Nkwera kujiuzulu bila kueleza kwa undani sababu za kujiuzulu kwake. “Ni kweli amejiuzulu nafasi yake, lakini siwezi kukupa maelezo yote kwa sababu niko barabarani naendesha gari,” alisema Mlote

Wafukiwa wakiiba madini Mirerani



 
WACHIMBAJI wadogo watatu wanasadikiwa kufa baada ya kufukiwa na kifusi, wakati wakiwa kwenye harakati za kuiba madini ya tanzanite katika mgodi wa Tanzanite One, Mirerani.
Taarifa ya kufukiwa kwa wachimbaji hao maarufu kama Wanaapolo, ilitolewa jana na mchimbaji mwenzao, Gidish Benedict (32), aliyekuwepo eneo la tukio na kunusurika wakati wenzake wakifukiwa.
Kwa mujibu wa Benedict aliyezungumza na waandishi wa habari mjini hapa, hajui kama wenzake watakuwa hai, kwani sehemu waliyokuwepo haikuwa na hewa hivyo kuna uwezekano wa wenzake watatu kufa wakiwa huko chini.
Aliwataja wenzake hao waliofukiwa kuwa ni Saidi Mgosi, mkazi wa Boma mkoani Kilimanjaro na wengine aliowataja kwa jina moja kuwa ni Dominic, mkazi wa Zaire Mirerani kwa jina la utani anaitwa Bwashee na Khalid, ambaye hafahamu anakotoka.
“Sijui kama wenzangu wapo hai au la maana nilimwambia mbona nguzo imebana sana, wakasema toka wewe si mzoefu wacha sisi wazoefu tufanye kazi. “Nilijibanza pembeni ya mwamba na kuwapisha watengeneze njia ili tutoke, lakini wakati wakigonga nguzo, udongo ulimwagika kwa kasi mimi nikarudi kwenye upenyo nikafanikiwa kupona, lakini sijui wenzangu kama wapo hai watakuwa wamefukiwa na kifusi,” alisema.
Amekiri kuwa walizama ndani ya mgodi huo Jumatatu ya wiki hii saa 7 usiku kwa njia za panya maarufu ‘bomu’, lakini wenzake wamefukiwa na kifusi na haijulikani kama wako salama.
*Tanzanite One
Akizungumzia jana Mirerani, Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Sky Associates, inayomiliki mgodi huo wa Tanzanite One, Apolinary Modest alisema Wanaapolo hao waliingia katika mgodi huo uliofungwa Jumatatu wiki hii na kuanza kuchimba madini.
Kwa mujibu wa Modest, baada ya kumaliza kazi hiyo walianza safari ya kurudi juu, lakini walishindwa kufika juu siku ya Ijumaa, baada ya kugonga nguzo ambayo ilitoa udongo mwingine uliosababisha njia hiyo ya panya kuziba.
“Hivi sasa tupo na wataalamu wetu wa uokoaji kutoka Afrika Kusini kwa ajili ya kuwaokoa Wanaapolo hawa ambao hatujui kama wapo hai au la. “Bado kama mita mbili au tatu kufika eneo la tukio chini ya ardhi ili kuona kama wapo hai au wamekufa au wamepita njia nyingine za panya na kukimbia,” alisema Modest.
Alisema njia za panya zipo nyingi na kampuni imejitahidi kuziba, lazini zinazibuliwa na Wanaapolo ili kuingia ndani ya mgodi uliofungwa au unaoendelea kuchimbwa madini hayo kwa nia ya kuiba madini.
Modest alisema machimbo yapo mengi zaidi ya 100 ambayo yamezibwa, lakini Wanaapolo hao wamekuwa wakizibua kwa njia zao na kuingia eneo la Tanzanite One, ili kuiba madini hayo na mchimbaji huyo aliye hai, anashirikiana na waokoaji kuonesha njia walizopita ili wenzake waokolewe.
Wanaowapeleka Shuhuda huyo, Benedict aliendelea kusema kazi hiyo ya kwenda kuiba madini, hufadhiliwa na wafanyabishara wakubwa wa madini ambao hutoa mamilioni ya fedha kwa wachimbaji hao ili wafanikishe wizi huo.
Alisema wao hawana nia mbaya, bali husukumwa na wafanyabiashara hao ambao hutenga mamilioni ya fedha kwa kazi hiyo. ‘’Sisi tunanunuliwa zana zote za uchimbaji na tunatumwa kwenda kuiba madini Tanzanite One na huko chini ni usalama wako ndio unakulinda na ukipata madini, unampelekea kwa aliyekufadhili ambaye ni mafanyabiashara mkubwa wa tanzanite.
“Naomba mnisamehe maana msukumo ndio unatufanya tufanye kazi hii ya bomu na njaa pia inachangia,’’ alisema. Kamanda wa Polisi wilayani Simanjiro, Francis Massawe amethibitisha tukio hilo na kuongeza kuwa bado wanaendelea na uokozi. Imeandikwa na Veronica Mheta na John Mhala, Arusha.

Waliochoma nyumba saba Pemba wasakwa


 
 
JESHI la Polisi limeanza msako wa watu waliochoma nyumba tano za wananchi wakazi wa Kangagani, ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Kituo cha Afya katika Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu kutoka Pemba jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Hassan Nasiri Ali, alisema watu wanaotafutwa wamechoma nyumba tano za wananchi, Kituo cha Afya cha Kiuyu Minungwini na ofisi ya CCM Tibirinzi.

“Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kuhusu matukio matatu ya hujuma za kuchoma moto nyumba za wananchi, kituo cha afya na ofisi ya Chama Cha Mapinduzi. Matukio hayo yote yanaonekana kuwa na muelekeo wa vitendo vya hujuma,” alisema.

Kamanda Nasiri alisema katika matukio hayo hadi sasa hakuna mtu anayeshikiliwa Polisi wala hakuna aliyejeruhiwa na Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kuhusu matukio hayo.

Mkuu wa Mkoa Awali Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Omar Khamis Othman alipiga marufuku mikusanyiko ya watu katika nyakati za usiku ikiwa ni sehemu ya kujaribu kupambana na kupunguza vitendo vya hujuma alivyosema vimelenga kuvuruga uchaguzi wa marudio unaotazamiwa kufanyika Machi 20 mwaka huu.

“Tumepiga marufuku mikusanyiko ya vikundi vya watu katika nyakati za usiku ili kupambana na matukio ya hujuma yanayofanywa zaidi katika kipindi hiki kuelekea katika uchaguzi wa marudio, ambao baadhi ya watu wanataka kuvuruga kwa makusudi na kuzuia haki ya wapiga kura,” alisema.
Awali Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai akizungumza kwa simu kutoka Pemba, alisema matukio hayo yamelenga kuhujumu na kutisha wananchi ambao ni wafuasi wa chama hicho, ili wasijitokeze kupiga kura katika uchaguzi wa marudio.

Akifafanua zaidi alisema matukio hayo yote yanaonesha waziwazi yamelenga wafuasi wa CCM kwa sababu hakuna mwanachama wa CUF, ambaye nyumba yake imeharibiwa na moto.
“Haya matukio yote yanaonesha wazi wazi kwamba ni sehemu ya vitendo vya hujuma kwa ajili ya kuwashambulia wafuasi wa CCM na kuwatisha ili wasijitokeze katika uchaguzi wa marudio’ alisema.
Vuai aliwataka wafuasi wa CCM kuwa watulivu katika kipindi hichi kigumu na kuviachia vyombo vya dola kufanya kazi yake ya uchunguzi na kuwatia hatiani watuhumiwa wa matukio ya hujuma, ambayo hivi sasa yamekuwa yakijitokeza kwa wingi Pemba yakiwalenga zaidi wafuasi wa CCM.

Wananchi wa Zanzibar wapo katika matayarisho ya uchaguzi wa marudio unaotazamiwa kufanyika wiki ijayo Machi 20 mwaka huu, ambapo Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec), tayari imeanza kutoa mafunzo kwa mawakala wa vyama vya siasa watakaosimamia uchaguzi wa marudio, ambao unafanyika baada ya kufutwa kwa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25.

Thursday, March 10, 2016

Wafanyabiashara wa soko la kwa Morombo wagoma kuhama

Wafanyabiashara wa soko la kwa Morombo wagoma kuhama



 

Mwenekiti wa mtaa wa FFU Bw Anaclet Edward
 




 Bi. Regina Makorongo akichochea moto
 



Mfanyabiashara wa soko la kwa morombo jijini Arusha Zena Shabaan
 Wafanyabiashara wa soko la kwa Morombo wamegomea manispaa ya jiji la Arusha kuhamimia katika eneo lililotengwa na serikali na kusema hawako tayari kutokana na miundo mbinu ya soko hilo kuwa mibovu na  kuhofia usalama wa mali zao
Hata hivyo amesema kuwa mtu anapokamatwa na manispaa anatakiwa apelekwe mahakamani na siyo mahali pengine  na kuiomba serikali  hii ya awamu ya tano iwatengenezee mazingira mazuri ya biashara
“Yaani hawa manispaa wanatunyanyasa kwa kweli, sisi kufanya biashara zetu pembezoni mwa barabara ni kutokana na mazingira ya soko ambalo walitupeleka kuwa mibovu na hakuna ulinzi wowote ambao utaweka hali ya usalama tunalipa kodi sasa hizo pesa zetu za kodi wanazipeleka wapi ?” Alisema mmoja wa wafanyabiashara
Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa  wa FFU  ambako linapatikanaa soko hilo Bw. Anaclet Edward amesema  kuwa eneo wanalofanyia biashara kwa sasa ni kinyume cha sheria  kwani mwaka jana walipewa barua ya maandishi wahame eneo hilo lakini cha kushangaza hadi sasa wapo wanaendelea na biashara 
Sanjari na hayo Bw. Edward ameongeza kwa kusema yeye hawanyanyasi wananchi  wake bali anatekeleza jukumu hilo kwa manufaa yao wenyewe
“Mimi nafanya hivyo kwa ajili ya kuwaweka kwenye usalama kwa siyo tu ni amri kutoka manispaa ya jiji letu hili cha msingi wananchi wafuate kanuni  na utaratibu unavyotaka”Aliongea mwenyekiti huyo