Showing posts with label HABARI ZA KIMATAIFA. Show all posts
Showing posts with label HABARI ZA KIMATAIFA. Show all posts

Wednesday, February 24, 2016

BESIGYE; NILIKAMATWA MARA NNE


Image copyrightAP
Image captionKiongozi wa Upinzani wa Chama cha FDC, Kizza Besigye

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Kiiza Besigye ameiambia BBC Kuwa ametiwa mbaroni na polisi mara nne kwa muda wa siku sita kufuatia uchaguzi uliofanyika nchini humo wiki iliyopita. Matokeo ya uchaguzi huo yalimpa ushindi Rais Yoweri Museven kutawala nchi hiyo kwa muhula wa tano.
Bwana Besigye ambaye yupo kizuizini nyumbani kwake ameeleza jinsi alivyokamatwa na polisi.
"nilikamatwa na polisi nikiwa nyumbani mwendo wa saa kumi na moja alfajiri, na kupelekwa kwa mwendo kasi mjini ambao ulikuwa ni mwendo wa kutisha ili kuwakwepa waandishi wa habari waliokuwepo katika eneo walinikamata, na hii ilkawa ni mara ya nne kukamatwa na polisi kwa muda wa siku sita."
Besigye amesema amesikitishwa sana kwamba jamii ya kimataifa haijaingilia kati suala hilo kwa niaba yake. Ameonya kwamba kama wanadhani Rais Museveni ameleta amani na utulivu nchini Uganda wajue wanafanya makosa.
"Amani na utulivu ni upande mmoja wa sarafu. Upande wa pili wa sarafu ni haki. Hauwezi kuwa na amani na utulivu bila haki. Na hii ndio hali halisi katika mazingira yetu ni kwamba kwa kifupi hakuna haki "alieleza

WANAFUNZI WALIOCHOCHEA WENZAO WAJISALIMISHA HUKO INDIA



Image captionMwanafunzi aliyewachochea wenziwe India
Wanafunzi wawili wa kihindi waliodaiwa kuwachochea wanafunzi wa chuo kikuu cha Jawaharlal Nehru kuandamana huko Delhi wamejisalimisha kwa polisi wenyewe.
Umar Khalid na Anirban Bhattacharya ni miongoni mwa wale waliokuwa wakitafutwa na polisi.
Kukamatwa kwa kiongozi wa muungano wa wanafunzi wa chuo hicho Kanhaiya Kumar, mapema mwezi huu ndiko kulikosababisha ghasia katika sehemu nyingi nchini India.
Baada ya Bwana Kumar kukamatwa, wanafunzi wengine ambao wametajwa kuhusiana na maandamano hayo walitoweka lakini wakajitokeza katika chuo kikuuu cha JNU siku ya Jumapili usiku.
Polisi hawakuingia katika chuo hicho lakini jumanne usiku Umar Khalid na Anirban Bhattacharya waliondoka katika chuo hicho kwa hiari na kujisalimisha kwa polisi.
Polisi hawaruhusiwi kuingia vyuoni bila idhini ya viongozi wa chuo,ripoti zimesema.
Polisi wamewata wanafunzi waliosalia - Ashutosh Kumar,Anant Prakash Narayan, Riyazul Haq na Rama Naga -kujisalimisha